Posts

Showing posts from August, 2017

Man united kumuiba Alexis Sanchez

Image
Manchester united wanafanya mawasiliano ya chini kwa chini na wakala wa Sanchez ili kufanikisha usajili wa kushtukiza kwa kuwapora wapinzani wao wakubwa katika jiji la Manchester klabu ya Manchester City ambao tayari wameshafanya mazungumzo nae. Alexis amekuwa njia panda katika dirisha hili la usajili baada ya kugoma kuongeza mkataba mpya katika klabu yake ya sasa ya Arsenal ili atue klabu mpya yenye kiu ya mataji na itayoshiriki klabu bingwa. Mourinho ni mshabiki mkubwa wa mchezaji huyo raia wa Chile lakini ni kazi ngumu kumsajili mchezaji kutokana na uwepo wa kocha Guardiola katika klabu ya Manchester city aliewahi kufanya kazi na mchezaji huyo katika klabu ya Barca. Sanchez ataelekea Man united kama mbadala wa Perisic baada ya kushindwa kumsajili kutoka Milan ya Italy inayokaribia kumuongezea mkataba hivi karibuni.

Evra atoa povu lake mtandaoni

Image
Mchezaji wa zamani Manchester ambae haishiwi na vituko mitandaoni Patrice Evra ameibuka tena mpya baada ya kuwaponda wanaomzarau akiwemo na mwalimu wake mwalimu wake aliemwambia kuwa huwezi soka kwa sababu wewe ni mfupi. Evra amezoweleka kwa kutumia video mbalimbali mtandaoni akisema maneno kama "I love this game" akimaanisha kuwa huu mchezo naupenda mara hii amekuwa tofauti baada ya kutuma video inayomuonyesha akiwa mazoezini huku akisema "usiwe na wivu japo walisema siwezi sasa nina vikombe zaidi ya 21 nimecheza fainali nyingi na nimeshinda japo nimepoteza nyingi lakini nimeshinda makombe mengi na bado nahitaji makombe mengi zaidi" na akimaliza kuwa "I love this game"

Taarifa mpya za klabu ya Manchester United

Image
                   Antoine Griezman Wakala wa zamani wa Griezman amefichua kuwa ilibakia kidogo kwa mchezaji kujiunga na klabu ya Man united baada ya klabu yake anayoichezea ya Atletico Madrid kufungiwa kutokusajili. Taarifa zikisema kuwa klabu zote mbili zilikubaliana usajili wa mchezaji huyo kwa dau la euro milioni 100. Ivan Perisic Mchezaji anaewindwa vikali na klabu ya Manchester United Perisic, 28, anategemea kuongeza mkataba na klabu yake ya Inter Milan baada ya timu hiyo ya jiji la Milan kugoma kuwauzia mabingwa wa kombe la FA na Europa Man United. Milan watamuongezea mkataba hivi karibuni ili kuwakatisha tamaa Mashetani juu ya kumsajili winga huyo machachari.                     Luke Shaw Beki wa kushoto raia wa Uingereza Luke Shaw anatarajia kuongezewa mkataba wa kuendele...

Leicester yataka kumsajili Smalling

Image
Leicester city inataka kumsajili beki wa Manchester, Chriss Smalling kocha wa Leicester tayari ameshamsajili beki wa Hull city, Harry Maguire, 24, alieitwa na timu ya taifa ya Uingereza hivi karibuni na sasa anataka kumchukua raia mwingine wa Uingereza, Smalling aliekosa nafasi ya kucheza mara kwa mara tangu atue kocha Jose Mourinho na kumsajili Baily anayecheza sambamba na Jones wameonyesha ushirikiano mkubwa kiasi cha kuifanya Man United ishindwe kufungwa goli hata moja katika michezo yake mitatu ya mwanzo huku ikijikusanyia magoli kumi katika mechi hizo na kukiwa bado na ingizo jipya anaecheza pia nafasi ya beki wa kati kama Smalling aitwae Lindelof raia wa Sweden hivyo kuzidi kuwa na nafasi finyu katika timu hiyo ya Mashetani wekundu. Kocha wa Foxes, Shakespeare anataka kuiongezea makali safu yake ya ulinzi kwa kumsajili beki huyo raia wa Uingereza anayeonekana kukosa nafasi katika timu hiyo ya Man united kwa sasa ili kuirejesha katika ushindani kwenye ligi kuu ya Uingereza. Je ...

Nataka kusajili mchezaji wa nne maneno ya Mourinho

Image
Kocha Jose Mourinho ameweka bayana kuwa anataka kusajili ingizo jipya kwa kumsajili mchezaji wa nne lakini hata hivyo amesema kuwa hana haraka na hilo na hatawashinikiza bodi kufanya hivyo licha ya kuwa tayari ameshawasali wachezaji watatu ambao ni Lukaku, Matic kutoka kwa mahasimu wao Chelsea na Lindelof kutoka Benfica. Alisema "Inawezekana hata dirisha lijalo la usajili nikampata mchezaji wa nafasi ninayoihitaji ili kukiongezea makali kikosi changu" Manchester united wanaongoza ligi wakiwa na point 9 na magoli 10 huku wakiwa hawajafungwa hata goli moja katika michezo yao mitatu ya mwanzo msimu huu.

Mou amuonya Anthony Martial

Image
Mourinho hakusita kummimiminia sifa mshambuliaji wake Anthony Martial baada ya kuonyesha kiwango kizuri msimu huu na kufanikiwa kufunga mabao mawili na assist moja katika michezo yake mitatu ya mwanzo ya ligi kuu ambapo miwili kati yao amekuwa akiingia ndani ya uwanja kama mchezaji wa akiba. Mourinho alisema "Nadhani kuwa unapokuwa na kipaji huwezi kukiacha kipotee unapojaaliwa kipaji inabidi ukitumie kipaji chako na kukiendeleza bila ya kukiacha kipotee kipaji hicho." "Nahitaji kuona zaidi kutoka kwake kwa sababu ana vitu vyote hivyo nafikiri ananielewa zaidi kwa sababu tuna uhusiano mzuri tu"

Mkhtaryan na record mpya dhidi ya Leicester

Image
Mkhtaryan aweka record baada ya mchezo wake dhidi ya Leicester kwa kutoa assist kwa mchezaji Rashford na kuwa mchezaji pekee kufanya hivyo kwa kutoa assist tano katika michezo mitatu ya mwanzo ambapo imekuwa ni haraka zaidi kwa mchezaji wa ligi kuu ya Uingereza kuwahi kufanya hivyo akiwa sambasamba na Ruel Fox wa Newcastle aliyefikisha pasi kama hizo za magoli tano katika michezo mitatu ya mwanzo tokea msimu wa 1994/95. Mkhtaryan alitoa pasi mbili katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya West ham kwa kutoa assist kwa wachezaji Lukaku na Martial na kuendeleza kazi yake hiyo katika mchezo uliofuata dhidi ya Swansea akitoa tena pasi mbili kwa wachezaji Lukaku na Pogba na akimaliza kazi yake kwa Leicester mara hii akitoa assist kwa Rashford huku Klabu ya Manchester ikifikisha magoli 10 katika michezo mitatu.

Tetesi za usajili Man united

Image
Tottenham na Inter Milan kwa pamoja zimeingia katika mbio ya kumuwania beki wa PSG na anaewindwa na Manchester united Sergi Aurier beki huyo wa PSG na Raia wa Ivory coast anahusishwa vikali na kujiunga na Man utd. Chanzo : La Parisien Klabu ya Manchester united inamfatilia kiungo wa Anderlecht aitwae Leander Dendocker. Mashetani hao wekundu wametuma scout ili kumfatilia kiungo ambae alifunga goli walipokutana na timu hiyo katika mashindano ya Europa League, mchezaji huyo kwa sasa ana miaka 22, Kocha wa united anamtaka kiungo huyo kwa msimu ujao. Lakini pia mchezaji huyo anawindwa na klabu za Leipzig na Ac Milan ya Italia. Chanzo : The Mirror                 Klabu ya Watford inataka kumsajili kinda wa Man utd Timothy Fosu-Mensah kwa mkopo kinda wa United mwenye uwezo wa kucheza kama beki wa pembeni,kiungo mkabaji na beki wa kati hatma yake kuamuliwa baada ya mchezo wa dhidi ya Real Madrid. Chanzo : Dail Mail       ...